Social Icons

Pages

Tuesday, June 12, 2012

Shopping...


            
(Photo courtesy of Fotosearch)
                   
Hello,
I know hua unafanya shopping za namna tofauti tofauti.... Na kama sio kila mara at least mara moja kwa mwezi. Shopping ya chakula, ya vitu vya nyumbani kama (mashuka, vyombo nk), shopping ya nguo, accesories nk. Sijui kama hua unaandika list ya vitu unavyoenda kununua or not. I always do. Kwa sababu nisipoandika najikuta nanunua vitu nisivyohitaji na kusahau vile muhimu.

Anyway hilo ni la siku nyingine. Kwa leo nataka niongelee watu ambao na wao wanafanya shopping, mara nyingi inakuwa wanawake wenzetu. Specifically wakati tunafanya shopping za nguo, accessories, viatu, nywele. Wapo ambao hawajui wanachotaka na wengine hawajui kuchagua. Kwa hiyo wanakua wanaotea kukuangalia waone unachagua nini kisha wanadandia na hata kudiriki kukunyang'anya mkononi. "Oohh jamani nilikua natafuta sana sketi ya rangi hii" au " "uuuwwiii yaani nimesubiria sana kupata nywele za namna hii" Kisha anajifanya anaangalia angalia anakibeba na kwenda kulipia. Wanakuacha wewe umetoa macho hujui hata kinachoendelea. Kwa kweli I dont like hii tabia kabisa. Why utumie macho yangu kuona vitu vizuri? Mie ishanikuta sana. So hua nikiwashtukia watu wa na namna hii nitazunguka tu kwenye hilo duka bila kuchagua kitu hadi waondoke. Manake watanizingua nijikute nagombana nao bure.
Kama hauko sure na unachohitaji kwa nini usimuombe msaidizi kwenye duka husika akusaidie? That's why wapo pale.

Hata kwenye Supermarkets mtu anakuja hajui alichofuata, anakufuata nyuma kama mkia, ukienda section ya chakula yupo nyuma yako, ya sabuni - huyu hapa, ya toys - bado yumo. Kila utachochukua na yeye anabeba. Na anaweza akakuuliza kabisa - eti hii shampoo ni nzuri eeh? Mie hua hata sijibu. Kwani alikua akitumia shampoo ya aina gani all through?
Anyway, yashakukuta? If yes ulifanya nini?
Funguka...

Kwa maoni Email me - barbshassan@gmail.com
or sms - +255 759 008500


Siku njema
xoxo

5 comments:

  1. That is such a wonderful pleace where you live guys! Africa is the most beautiful continent ever!

    ReplyDelete
  2. haa unachekeshaje. hiyo ni roho mbaya fulani kwa sababu mi sioni kama kunatatizo mtu akipenda ulichochukua wewe. we huoni kama vitu vya dizain hiyo ni vingi na siyo single sasa visiponunuliwa utanunua wewe let say set ama dozen yote?usiwe na roho ya ubinafsi

    ReplyDelete
  3. jamani wanawake tusibaniane, ndo maana unakuta mtu kavaa vibaya unamwambia umependeza.. kumbe mwenzio kachemsha mbaya, bora umsaidie mteja mwenzio bana tuache roho mbaya. mm sipendi kuwauliza wztu wa madukani kabisaa coz wananitenda sana ni hawa hawa wanawake wenzetu, atakuambia kitu ni kizuri ili ununue alafu kumbe hakikufai, ye anafanya biashara..... mm nina vitu vingi home sijavitumia sababu ya hawa watu unanua ukivaa wanaokupenda wanakuambia hamna hapa ulichemka, tusaidiane jamani... tena hii mada muhim saaaaana

    ReplyDelete
  4. Kumbe na wewe una roho ya choyo du!i thot ungemsaidia na kua proud kwa kua unawexachagua kitu kinachopendwa na wengi kumbe ni unadiriki kisema utazunguka tu kuliko mtu akufatefate. No wonder God gave u that shape na lisura bovu kumbe hata roho yako mbayyyyaaaa

    ReplyDelete
  5. samahani lakini kama ntakua nimekosea ila kiukweli unakosea kufanya hivyo dada! maana kuna baadhi ya wanaokuuliza hukuuliza kwa nia njema na safi kabisa wakiamini kua wewe utakua na choice nzuri coz ni mtu maarufu na sister duu,so si vbaya kumshauri mtu pale anapoomba ushauri wako..

    ReplyDelete

 

Sample text

Sample Text

Sample Text