Social Icons

Pages

Monday, December 17, 2012

KOFII OLOMIDE ASHUSHA BURUDANI NZITO UWANJA WA CCM KIRUMBA USIKU HUU

Kofii Olomide na Mwimbaji Cindy wakiimba huku wakiwa amezungukwa na wanenguaji wake
Mwanamuziki Kofii Olomide akipanda jukwaani huku akisinddikizwa na waimbaji wake.
Cindy katikati Mwimbaji mahili wa kike wa mwanamuziki Kofii Olomide akiimba jukwaani kalba ya Kofii Olomide mwenyewe kupanda jukwaani.
Kazi iko hapa kama wanavyoonekana wanenguaji hao wakicheza kwa sataili ya aina yake.
Hii ilichezwa kwa kwenda mbele na kurudi nyuma huku wakiwa wameshikana.
Palikuwa hapatoshi kwa shoo kabambe kabisa kutoka kwa wanenguaji wa Kofii Olomide.
Ili mradi burudani iliyopangika kutoka kwa wanenguaji hao
Staili hiyo ilichezwa kwa hisia pia
Kutoka kulia ni Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa  (SBL), Anitha Msangi Maurice Njowoka na Patrick Kisaka kutoka kampuni ya bia ya Serengeti wakishoo love kwa picha.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti Ephraim Mafuru kulia na Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga wakiwa katika picha ya pamoja
Wadau kutoka Miss Tanzania wakiwa katika onesho hilo.
Rachel wa THT akicheza na mmoja wa wanenguaji wa mwanamuziki Kofii Olomide.
Kofii Olomide akimpongeza msanii Rachel wa THT baada ya kuonyesha uwezo wake katika kuimba kwenye onesho hilo.
Waimbaji wa mwanamuziki Kofii Olomide wakiimba kwa hisia katika enesho hilo.
Rapa wa mwanamuziki Kofii Olomide anayejulikana kwa jina la Computar akighani huku wanenguaji wa kiume wakiingia jukwaani.
Jukwaani ni Recho wa kundi la  THT kutoka jijini Dar es salaam akinendelea kutoa burudani jukwaani
H. Baba akifanya vitu vyake mbele ya mashabiki wa jijini Mwanza wakati akitoa burudani ya utangulizi kabla ya mwanamuziki Kofii Olomide Kupanda jukwaani.
Pepe Kale wa Mwanza naye akafanya mambo makubwa na kukubalika na umati wa mashabiki waliohudhuria katika onesho hilo.
Wasanii wa Kundi la THT wakitumbuiza katika onesho hilo.
Bendi ya Hill Way ya Mwanza ikitumbuiza katika utangulizi
Kundi la Hill Way Band likifanya vitu vyake jukwaani katika utangulizi wa burudani za tamasha la Tusker Carnival kabla ya mwanamuziki Kofii Olomide kupanda jukwaani.
Mashabiki wakiwa wameanza kumiminika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mashabiki wakiwa  kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakisubiri kuona burudani ya Kofii Olomide.
Haya ni maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya kujipatia bia yako ya Tusker Lager na vinywaji vingine vinavyotengenezwa na Kampuni ya bia ya Serengeti
 
Haya ni maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya kujipatia bia yako ya Tusker Lager na vinywaji vingine vinavyotengenezwa na Kampuni ya bia ya Serengeti

Monday, June 25, 2012

Hook Me Up....


                                           

Hellow....
Kwema? How was the weekend? Yangu ilikua poa tu nashukuru.. Nililala weekend nzima! Nimekuja ofiisini asubuhi nikiwa sooo refreshed...
Anyway I know wanawake wote tuna girl friends, mashosti wengi wengi tu, wengine tuko nao closer kuliko wengine. Na pia kwa vile mie ni mwanamke na pia nina friends nina uhakika yatakuwa yameshawahi kukutokea haya. When una boy friend, na shosti wako yuko single - wengi wao hua wanaomba uwa hook up na rafiki za boy friend wako, au hata labda na kaka yako, uncle na kadhalika!
What do we expect? Labda hua tunadhani kwa vile labda your boy friend ana vigezo na tabia njema then marafiki zake pia watakua the same? Au tunataka kuunganishwa (kua hooked up) ili twende on double dates?
Personally, all the hook ups ambazo nishawahi kupata hazikufaa. Nilikimbia mwenyewe!!! Wanakua sio what you expected...

Hii ni tabia ambayo wanawake wengi tunayo, tusidanganyane... Swali ni kua - does the relationship work hata ukiwa hooked up? Ishawahi kutokea kwako na upo na huyo mtu till now? Au iliishaje? Ningependa kujua tu.... Let's share...

Funguka...

Email me - barbshassan@gmail.com
or SMS -0 +255 759 008500

xoxo

Thursday, June 21, 2012

Mamaangu ni Rafiki Yangu...


                                       


Mambo zenu?
Personally mimi sikupata bahati ya kuwa karibu na mamangu mzazi kwa sababu alifariki nikiwa mdogo, ila nililelewa na bibi (mamake mama) na mama mkubwa. Ambao hawa walinilea kama mwanao kabisa na mimi nikawapenda, kuwaheshimu na kuwa karibu nao kama mama zangu kabisa. Kile ambacho ningetakiwa kumwambia my mum nilikua nawaambia wao, na kile ambacho nilitakiwa nimpe mama yangu niliwapa wao. Niliwaonea sana wivu wale waliokua wakipeta na mama zao wazazi, akija shule "mamangu hivi, mamangu vile."  But nilizoea baada ya muda.
Anyway my point kwa leo ni kuwa my son sikuweza kua karibu naye kwa sababu I was busy na chuo na kazi. Mara nyingi nilikua sipo nyumbani. Yeye akawa close to my kid sister Eugenia. Hapa pia nikawa na wivu, nilitamani kweli niwepo home mara nyingi ili niwe closer to my son. Lakini nilikua namtafutia future kwa hiyo nikavumilia tu.
Baada ya kupata mtoto wa pili Ashley, nikasema hapa ndipo. Huyu sasa kaja wakati I'm settled, so nitajaribu niwezavyo kuwa very close to her. Na imetokea hivyo. Wanasaikolojia wanasema kuwa wakati wa kutengeneza bond na mwanao kama mzazi ni toka akiwa mdogo. Akishafikisha miaka 12 kama hakuna bond basi sahau. Right now nashukuru Mungu because my daughter ananiambia kila kitu, chochote anchowaza, chochote anachopitia. Yaani akitoka shule tunakaa chini anaanza kunielezea ilivyokua shule siku hiyo, what she learned, marafiki zake, walimu wake, ananiimbia. Na usiku kabla hatujalala anasali with me, ananiambia hadithi za shule - au mara nyingine mi ndo namuelezea. She wants to know about my colleagues at work, kama nina vikao the next day, yaani ratiba yangu nzima. Wakati she is only 5. Sio kua najisifia but namshukuru tu Mungu kua at least - baada ya kukosa kuwa close na mama mzazi, my kid sister na my son - Mungu amenipa another chance.
Je wewe, mama yako ni rafiki yako? Hua munaenda saluni pamoja? Harusini? Munapika wote? Munapiga story/umbea? Je, hua unapata chance hata kwenda for dinner wewe tu na mama yako? Kuongea about maisha ulikotoka na unapokwenda? Na siongelei right now tu ila hata zamani wakati unakuwa. Kiukweli hakuna rafiki kama mama, mama aliyekuzaa, mama aliyekupa unconditional love, mama atakaye stand by you hata kama wewe umekosea, mama atakayesimama katikati pindi baba anapotaka kukuchapa, mama anayeweza kufa kwa ajili yako.
Tuwape mama zetu chance ya kuwa close na sisi, na hata kama hukuweza kufanya before na bado yu hai, unaweza kuanza sasa. And from her utaweza kujifunza how to be close to your own children.
Kwa leo ni hayo tu... Nimetoa yangu ya moyoni...

xoxo

Kwa maoni au story yako - Email - barbshassan@gmail.com
or SMS - +255 759 008500

Wednesday, June 13, 2012

Jamani - Balaaaa

Jamani jamani.. Mimi kama mwanamke wakati namnyonyesha mwanangu nilikua naona aibu kutoa nyonyo mbele za watu. Sasa imajin na utu uzima huu eti nimtolee mwanaume nyonyo hadharani anyonye kwa raha zake. Coz kwake sio chakula!!! HAHhhhahahahah..
Kumeingi mtindo huu mpya nchini Ghana wakaka watanashati wadogo wadogo kiumri wakienda out kwenye clubs wananyonya maziwa ya madem zao nje nje bila aibu!
Swali - I know hao wanaume hawataona aibu kihivyo, lakini kwa wadada je? Na hizo night clubs kwa nini wasiwakatalie kufanya hivi?
Je, wewe unaweza kuthubutu to do the same?

Have a lovely day,
xoxo

Maoni Email - barbshassan@gmail.com
SMS - +255 759 008500

Tuesday, June 12, 2012

Shopping...


            
(Photo courtesy of Fotosearch)
                   
Hello,
I know hua unafanya shopping za namna tofauti tofauti.... Na kama sio kila mara at least mara moja kwa mwezi. Shopping ya chakula, ya vitu vya nyumbani kama (mashuka, vyombo nk), shopping ya nguo, accesories nk. Sijui kama hua unaandika list ya vitu unavyoenda kununua or not. I always do. Kwa sababu nisipoandika najikuta nanunua vitu nisivyohitaji na kusahau vile muhimu.

Anyway hilo ni la siku nyingine. Kwa leo nataka niongelee watu ambao na wao wanafanya shopping, mara nyingi inakuwa wanawake wenzetu. Specifically wakati tunafanya shopping za nguo, accessories, viatu, nywele. Wapo ambao hawajui wanachotaka na wengine hawajui kuchagua. Kwa hiyo wanakua wanaotea kukuangalia waone unachagua nini kisha wanadandia na hata kudiriki kukunyang'anya mkononi. "Oohh jamani nilikua natafuta sana sketi ya rangi hii" au " "uuuwwiii yaani nimesubiria sana kupata nywele za namna hii" Kisha anajifanya anaangalia angalia anakibeba na kwenda kulipia. Wanakuacha wewe umetoa macho hujui hata kinachoendelea. Kwa kweli I dont like hii tabia kabisa. Why utumie macho yangu kuona vitu vizuri? Mie ishanikuta sana. So hua nikiwashtukia watu wa na namna hii nitazunguka tu kwenye hilo duka bila kuchagua kitu hadi waondoke. Manake watanizingua nijikute nagombana nao bure.
Kama hauko sure na unachohitaji kwa nini usimuombe msaidizi kwenye duka husika akusaidie? That's why wapo pale.

Hata kwenye Supermarkets mtu anakuja hajui alichofuata, anakufuata nyuma kama mkia, ukienda section ya chakula yupo nyuma yako, ya sabuni - huyu hapa, ya toys - bado yumo. Kila utachochukua na yeye anabeba. Na anaweza akakuuliza kabisa - eti hii shampoo ni nzuri eeh? Mie hua hata sijibu. Kwani alikua akitumia shampoo ya aina gani all through?
Anyway, yashakukuta? If yes ulifanya nini?
Funguka...

Kwa maoni Email me - barbshassan@gmail.com
or sms - +255 759 008500


Siku njema
xoxo

Thursday, June 7, 2012

Women In Balance...

Usipitwe mdau wa wanawakenisisi. Haya si ndio mambo yenyewe sasaaaa... See you!!!!

XOXO

Kwa maoni - Email me - barbshassan@gmail.com
or SMS - +255 759 008500

Monday, June 4, 2012

Nisaidie...


                                        

Hello Barbara,
Im sorry na share nanyi stress zangu jumatatu.. But sikujua nitapata wapi usaidizi. Mi ni mdada nimeolewa na nina watoto wawili wavulana. Mmoja ana miaka 7 na mdogo ana miezi 8. Naishi na mume wangu pamoja na mtoto wa babangu mdogo (cousin wangu) ambaye hunisaidia kazi za nyumbani ila hua namlipa mshahara.
Amekua akifanya kazi vizuri tu, kunisaidia kulea wanangu na hata kuwasaidia na homework pindi ambapo mimi na mume wangu tunachelewa kufika nyumbani.

Juzi ijumaa cousin wangu alitoa kali ya mwaka. Mimi pamoja na mume wangu tulikua kazini, na mwanangu wa kwanza alikua shuleni. Cousin wangu alibaki na mtoto mdogo kama kawaida. Cha kushangaza niliporudi  nyumbani mida ya saa 10 na nusu nilikuta mlango wa nyumbani ukiwa wazi. Nikaingia nikamuita cousin yangu bila majibu. Kuingia chumba cha watoto nikamkuta mwanangu mdogo kalala kwenye kitanda chake akiwa mwenyewe na wa moto ajabu. Amejikojolea, kujinyea na machozi yamekauka katika macho yake.

Nikaenda kwa jirani kuuliza kama wamemuona dada, wakasema aliondoka toka asubuhi. Si ndo mie kushtuka. Dada wa nyumba ya jirani akanambia amemuona bar ya jirani. Na wakasema wamemskia mwanangu akilia siku nzima. Imagine mtoto wangu kumbe alikua hajala, hajaogeshwa, hajabadilishwa pampers siku nzima. Nilisikitika sanaaaa. Nikampikia mtoto na kumlisha, nikamuogesha akalala. Nikakaa kumsubiri dada, aliingia nyumbani saa 12. Yuko njwiii kalewa balaaa...
Hivi kweli angenambia nini nimuelewe? Alishindwa nini kununua pombe na kukaa anywe ndani ya nyumba huku akimuangalia mtoto? Ni unyama wa namna gani huu?
Sasa leo nimeshindwa hata kwenda ofisini niko nyumbani. Sijui nitaanzia wapi kutafuta dada mwingine. Naomba please wadau wa blog hii munisaidie..

Claire
Dar Es Salaam..

Friday, May 25, 2012

Nifanyeje???


                                           

Shikamoo Dada Barbara,
Naitwa Lucy ni msichana wa miaka 23 na nipo chuo mwaka wa pili. Natokea katika family ya middle class na mama yangu ni single parent. Sijawahi kumfahamu wala kukutana na baba yangu. Nina boy friend ninayempenda sana na tumekuwepo kwenye mahusiano kwa miaka 2 sasa. Nilikutana naye chuoni. Na ndio nashiriki naye kimapenzi.
Mwezi jana mama yangu aliniita nikakaa kitako akidai ana mambo anata ku discuss nami. Ila alichoniambia kwa kweli kimeni frustrate sana na nipo njia panda sasa hivi. Mama alinambia kwa sauti ya upole na iliyojaa majonzi kuwa " Yeye ni muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi na alibeba mimba yangu wakati ameshaathirika bila kujijua." Kwa hiyo ina maana mimi ni carrier wa HIV. Aliniomba nimsamehe kwani anahisi ameniharibia maisha yangu. Sikua na cha kumjibu na sijapata hadi sasa hivi. Nilienda kupima ili kuthibitisha na kweli nikakuta mimi ni muathirika. Sijui cha kufanya na mawazo yamenijaa tele. Na huyu kaka wa watu - my boy friend nimeshafanya naye mapenzi mara nyingi tu bila kutumia kinga. Naanzia wapi kumwambia hali yangu? Nahisi ataona mimi nilikua naifahamu hali yangu all through and chose not to tell him. Si ataona nilikusudia kumuua?
Katika chuo ninachosoma kuna a counselling center nimekua nikishinda humo kwani nimechanganyikiwa kabisa!
Naomba msaada wako wa kimawazo - na pia kutoka kwa wasomaji/ wadau wa blog hii..

Mubarikiwe
Lucy...

                                 
PS. Kwa leo sina comment. Nakuomba wewe mdau wa blog yangu tumsaidie Lucy...


Tuesday, May 22, 2012

Hereni....

                           

                                      



Mambooooo.. Kwema?
Nina swali.. Je before ununue earings hua unangalia nini?
Urembo, kama ni Unique, bei au uzito??? Mimi binafsi cha kwanza kabisa naangalia urembo - kama they are attractive na cha pili ni uzito. Umeshawahi kununua hereni and then later on unashindwa kuvivaa because ni vizito kupitiliza? Hereni nyingine zinakua nzito kiasi cha kuwa inatanua kale katundu ka skio. Ishawahi kukutokea? So umeamuaje? Urembo kwanza au uzito kwanza? Hehheheheh. Urembo taabu jamani..

Hebu angalia jinsi skio linavyovutika...... Pindi unapovaa heavy or wide earings...

 Aisee hata kama ni fashion - acha niiitwe mshamba....


 mmmhh...



 Hapanaaaaaaa.....



                             
Nisijeishia kua na maskio ya hivi..


Things to consider wakati wa kununua hereni.

- Material - zimetengenezwa kutumia material ipi? (plastic, silver, chuma) Ukizingatia what are you are allergic to...
- Uzito - Zitavuta maskio yako?
- Upana - Zitatanua kitundu cha skio?
- Unique - unique badala ya fashion (this is my motto) Although wengine wanaangalia how sexy they are au kama zipo in fashion.

Karibu kuongeza maoni yako...

Contact me:
Email - barbshassan@gmail.com
SMS - +255 759 008500

Thursday, May 17, 2012

Tatua Thursday....


                                                                       

Mambo Barbara,
Najua fika kua hua unapokea na ku post zaidi matatizo ya wanawake, ila hata sie wanaume tuna matatizo yetu... Na ndicho kilichopelekea mimi kukuandikia leo hii. Naitwa James, na nipo katika mahusiano na a beautiful lady ninayempenda sana na nia yangu ni kufunga naye pingu za maisha one day.
Tatizo linakuja kua mimi napenda sana sana kukiss. Nilijifunza kukiss baada ya kuona kwenye vipindi kwenye tv na kwenye movies. Nikaanza kujifunza  kujikiss mwenyewe kwenye kioo, mara nyanya au chungwa. Hadi nilipojiamini kua sasa najua ndo nikaanza kukiss ladies. Wazungu wanasema practice makes perfect - najiamini sasa hivi mimi ni bingwa wa mabusu. Tatizo langu ni kua my girl friend hajui kabisaaaa kukiss, na wala hana interest ya kutaka kujifunza. Mimi inaniwia ngumu sana sana. Manake ni kitu ninachopenda zaidi kufanya, in fact napenda zaidi kukiss kuliko sex. Ila mwenzangu na mie yaani wala, nikifuata midomo yake ya juu yeye ananitolea ulimi na akiwa amejaza mate kibaooo. Sina kinyaa ila inaboa.
Munanishaurije?
Je - nimuache na kutafuta a lady anayejua kukiss?
Je - nimvulie tu - ila itaniuma sana
Au ning'ang'ane kumfundisha tu - although hana hata mpango wa kutaka kujua kukiss.
Naomba msaada please.

Regards,
James

Kwa kweli wengi tunachukulia kissing poa - ila I'm one of those people ambaye napenda sana sana kukiss..  My first experience ya kukiss huyo jamaa alikua kala vitunguu! Aiseee nilichukia kissing kwa muda mrefu sana. Hadi nilipopata mtu ambaye alinifanya nipende kissing. Right now hunambii kitu!! Hahahhah. Experience yako ya kissing ikoje? Unapenda why? Na kama hupendi why? Na kama hujui - je unafanya nini ili kujifunza?  Manake wenzetu wanasema - Kissing is opening the window to someone's soul.
Funguka na pia tumsaidia James... Maoni yako ni muhimu sana...


                                         
mwaah!!!
have a great day

Thursday, May 10, 2012

Mothers Day.....


                               



Hello...
Siku tunayo feel special, ku feel tunapendwa na kua appreciated kama kina mama inawadia.. Ni 13th May - Mothers Day...
Aunty Sadaka ameandaa event itayotufanya tuji feel more special sisi kama kina mama na familia zetu..

" To celebrate mothers day, Aunty Sadaka ame organise a special event kusherehekea motherhood. All mothers na kina baba wanakaribishwa. Mlete mama yako, aunty, sister na any significant woman katika maisha yako at JB Belmont this saturday 12th May for dinner, dance na special activities. Show your appreciation to this special woman in your life kwa Tsh 50,000 kwa kila mmoja.

A CHILD"S BEST FRIEND IS THEIR MOTHER....

USKOSE....

Pata ticket yako mapema at - Shear Illusion - Mlimani City au Nyumbani Lounge au piga namba - +255 655 717575 au +255 787882


hugs
xoxo

Tuesday, May 8, 2012

Saidia Kutatua Tungo Hii......


                                                             
BABRA MIMI NI MWANAMKE WA KITANZANIA IMEOLEWA NA NINA MTOTO MMOJA  WA KIUME NA MUME WANGU JAPOKUA AMENIKUTA NA MTOTO MMOJA WA KIKE. TULIKUBALIANA NA HANA TATIZO LA KUMLEA BINTI YANGU.
MAHUSIANO YETU YALIANZA KAMA UTANI, MUME WANGU NILISOMA NAYE SHULE YA MSINGI! LAKINI TUKAJA KUPOTEZANA KWA MIAKA MINGI, LAKINI NIKIWA WAKATI WA MCHANA NA RAFIKI YANGU  KWA AJILI YA CHAKULA CHA MCHANA AKAPITA. NIKAMWAMBIA RAFIKI YANGU! "MH HUYU KIJANA NAHISI NAMFAHAMU"  AKATUPITA BILA KUJUA. ALIPOFIKA MBELE KIDOGO, NIKAMWITA NA KUMKUMBUSHA, AKAFURAHI KWELI. NILIPOTAKA KUJUA ANAKOELEKEA, AKANITAJIA JINA LA OFISI YETU, NIKAMUULIZA KULIKONI? AKAJIBU AMEAJIRIWA HUKO.
BASI MAISHA YAKAENDELEA KAMA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI MOJA, WAKATI HUO NILISHAACHANA NA BABA WA MTOTO WANGU WA KWANZA.BASI BINADAMU AMEUMBWA NA HISIA! TUKAANZISHA MAHUSIANO YA KIMAPENZI. LAKINI KATIKA KAMPUNI HIYO HIYO KUNA MWANAMKE ALIKUA ANATAFUTA MTOTO, BILA KUTEGEMEA KWA SIRI WAKAANZISHA UHUSIANO! LAKINI MTU HAKUNYIMI NENO, NIKATONYWA, WALAKINI SIKUTILIA MAANANI NA WAKATI HUO MIPANGO YA NDOA ILIKUA INAENDELEA, SO NILIJUA NI NJAMA NA HILA ZA WALIOKUWA HAWANITAKII MEMA, KUMBE KWELI.
BASI, WAKATI NDOA INANUKIA NAMI NLIKUA NI MJAMZITO, NIKASIKIA YULE DADA NAYE MJA MZITO, SI NIKAULIZA KWA MUME? AKAKATAA KATA KATA, NIKAMWAMBIA NI BORA UWEKE MAMBO SAWA SASA HIVI, AKAENDELEA KUSHIKILIA MSIMAMO WAKE. NIKAACHANA NALO. KUMBE WENZANGU WANAENDELEA KWA SIRI NA MTOTO AKAZALIWA WA KIUME KAMA WANGU NA ANAFANANA NA BABA YAKE NA NIKASIKIA TENA HUWA ANA KWENDA KULE NA HULALA PIA!
DUH! BASI SIKUAMINI! MARA ZIKAANZA SAFARI ZA KWENDA MARA HUKU AU KULE! AMA ANASINDIKIZA MSIBA, MARA OH NILIKAMATWA NA POLISI ANARUDI ALFAJIRI, MARA ANIRUDIE NA T-SHIRT TOFAUTI UKIULIZA OHH NLOVAA ILIMWAGIKIWA NA KITU NIKANUNUA NYINGINE YA MTUMBA. SAWA SASA HIYO CHAFU IKO WAPI TUFUE, OH NILIITUPA! UKIWA MUONGO UWE NA KUMBUKUMBU, SIKU INGINE ALIPOKWENDA KULE AKAACHA ALICHOVAA AKARUDI NA ILE TSHIRT ALO DAI KAITUPA! NIKAMUULIZA! NIKAZUNGUUSHWA! NIKASHIT
MBAYA ZAIDI MAMA MKWE ANA MSHADIDIA YULE WA NYUMBA NDOGO! NIKAWA NAZIDIWA NA TAARIFA ZA MUME WANGU KUA ANAZIDI KWENDA KWA HUYO DADA MPAKA WALIOKUA WANAMUONA WANANIONEA HURUMA! NIKAITWA TENA NA TENA NIKAAMUA KWENDA. NIKIWA NJE NASUBIRI ATOKE NIMDHIHIRISHIE KUWA ULICHOKUA UNAKATAA MI NAJUA UKWELI WOTE, KULE NDANI NIKAWA  NAPEWA TAARIFA ZOTE ZA KINACHOENDELEA, SASA WAPO SITTING ROOM,SASA WAMEINGIA CHUMBANI, SASA WAKO BAFUNI, SASA WAMETOKA SEBULENI,MARA NIKAELEZWA NDO WANATOKA HIVYO NIWE TAYARI. BASI NIKASOGEA KARIBU NA MLANGO NIKASIKIA WANAVYO AGANA,KWA MABUSU TELE TELE, MTOTO NAYE AKAWA ANAELEKEZWA KUMBUSU BABA YAKE ANAONDOKA! YOTE NAONA NA KUSIKIA JAPOKUA WAO WALIKUA HAWANIONI.
NIKAONA INATOSHA NATAKA WOTE WAJUE NINAJUA KILA KITU, WALISHTUKA NUSU WAANGUKE! MTOTO AKAKIMBIZWA NDANI, MUME ALIKUA HAAMINI MACHO YAKE, NIKAMWAMBIA MUME  WANGU HAPA NDIPO ULIPO AGA KUA UNAKWENDA? MAJIBU YALIKUA MAGUMU.
NIKAAMUA KUWAACHA NIKAONDOKA ZANGU, KIUKWELI HAIKUA RAHISI NILIKUA NALIA KILA SIKU NA  KULA CHAKULA HAKIPITI. PRESSURE NA KILA KITU KIBAYA KILINIELEKEA MIMI. ILA NILIYASHINDA YOTE. KWA SASA NA JIONEA KAWAIDA TU AENDE AMA ASIENDE POA TU, NA TAARIFA ZAKE NAPATA ZOTE NAPATA.
LUCY
PS - Rukhsa kumshauri Lucy. Ingekuwa wewe Ungefanyaje????

Ukiwa na story yako nitumie - email - barbshassan@gmail.com
au SMS - +255 759 008500

Wednesday, May 2, 2012

Ulikutana na Mume au Boyfriend wako wapi?

Mambo,
Pole sana kwa kuwa kimya for a while.. It's a long story.... Ila naomba radhi kwa hilo... I was thinking, unajua jinsi mashangazi na wazazi wetu wanavyotulazimisha kwenda maharusini? Especially kwa sie ambao hatujaolewa. Wakiamini kuwa huko ndio tutakutana na "potential husbands" Sijui kama kuna ukweli wowote ndani ya hili. Anyway nikaona si vibaya tupeane advice kuhusu wapi tunaweza kukutana na hao "potential husbands". Na tunaweza kufanya hivyo kwa wewe ku share ni wapi ulikutana na aliye mume wako au boyfriend wako kwa sasa... I believe itasaidia sana.. Hehehehhehe
Je mulikutana club au bar? Ila hua wanasema eti ma boyfriend utakaoanzana nao club hawadumu


Au harusini?

Courtesy of www.8020fashions.blogspot.com

au kwenye funeral?

         
Airport?



Ndani ya bus au train?

                             
Au ofisini?

                                           

Fungukaaaaa.. Hehehehehe..

For a private neno niandikie - barbshassan@gmail.com
or SMS - +255 759 008500

much love
xoxo

Thursday, April 19, 2012

Mzigo Mpya Navo's Choice - Part 2






                             
                                         corset.... bana tumbo when wearing dresses.. :)




                         bwangaaaaa.. yep zimerudi....


                                        
                                           Kwa wewe uliokua unauliza nanunua wapi dresses... haya kazi kwako.... Navo's Choice karibu na Barclays Bank Mikocheni branch..

xoxo
 

Sample text

Sample Text

Sample Text