Social Icons

Pages

Thursday, November 10, 2011

Relationships (part 3)

Hello,
Nakua mkweli leo. I have never lived na mwanamume maishani mwangu, sipendi kitchen party at all! But all in all mamangu (Magdalena Mkunde) amenifundisha mengi kuhusu maisha na jinsi ya kujitegemea - whether naishi na mwanamume or not. Why nimeanza like this unajiuliza?
Well - Hua wanasema "The way to a man's heart is through his stomach" Hawakukosea. Kwani nani hapendi msosi? Na dont ask me kama - naishi nile au nakula ili  niishi (this is debatable)....
Imajin this - Mumeo/ stay in boyfriend wako kaenda ofisini siku nzima anarudi home humuangalii hata mara mbili - kisha to top it up unampikia wali na mchuzi wa mayai!! Mchuzi wa mayai unaujua? Im not talking about egg soup ile ya chinese! Nooo!! Mchuzi wa mayai!! Yaani unachemsha mayai pembeni. Kisha unakaanga mchuzi pembeni (ambao uko maji maji meupe kama mchuzi wa jela) kisha unamenya yale mayai ulochemsha unakata slices na kudumbukiza kwenye mchuzi!! Na hii unampikia 3 times a week!!! Hiviii huyu mwanamume akitafuta nyumba ndogo yenye kumliwaza na kumpikia mapochopocho utalalamika? Au ndo diet? Heheheheheh! Seriously!!!

                                    Bleeee (kama naniliu eeh)

Pamoja na hilo hujui kupika unaamua kupika ndizi matoke - unadumbukiza ndizi nzima nzima kwenye sufuria, unakatia onions na nyanya humo humo na nyama kidogo kisha unajaza maji hadi juu!! Vitunguu vyeupeee!! Huyo bwana si ataenda kula chips vumbi jamani!! Unamkosa hivi hivi ukiona na kumsogeza mbali nawe.
Plus unathubutu kumpa your house help vinasa (underwear) za mumeo afue yeye!! Hivi kweli??? Hivi ukiibiwa utamlaumu nani? Utaimba Mulika Mwizi hadi uchoke!!!
And these things sio lazima ukafundwe kuvijua ni logic tu!
Hebu imajin mume akirudi home unamhug and welcome him home, unamtayarishia maji ya kuoga (sio lazma umtilie asmini), muwekee his pajamas tayari. Then mkaribishe mezani ambapo unapika at least vitu vinne tofauti mf - wali, chapati, mchuzi wa kuku/samaki, na mboga za majani, salad and fresh juice. Kaa ule naye huku mkipiga story. Asking him siku yake ilikuwaje and stuff. Au nakosea? Mi ni hopeless romantic eeh? But ni vitu that I believe in jamaniii...

                                        
Anyway, kama hujui kupika basi jifunze at least vitu ambavyo your man likes. Na kupika sio rocket science anyone anaweza kujifunza.
Anyway ndo hivyo - I've thrown my 2 cents advice hapo ambayo hata mie mwenyewe ntajaribu kuifanya na kuikariri siku ya siku when I start living with a man.
Ila jamani if the man pia mara moja moja akikupikia - rahaaaaa eeh? Hehehehe...

Have a lovely day
xoxo

13 comments:

  1. huyo anayepika vyakula vya aina tatu atakuwa mama wa nyumbani au nae anafanya kazi,maana na hizi foleni wote mnafanya kazi inawezekana mkawa mnapitiana mnakaa kwenye foleni saa tatu ndio mnaingia home jee hapo utaweza kupika vyakula vya aina Tatu,ifikie mahali tusiwabembeleze sana wanaume zetu waendane tu na hali halisi ya maisha, unaweza ukajitahidi kujipanga umfanyie kila kitu still bado akatoka maisha ni maelewano tu kama mtu anakupenda hata mboga ya mayai ukiiunga kwa nazi inalika vizuri.

    ReplyDelete
  2. Hi MS Babra
    Kuna ninavyokubaliana na ww na nisivyo kubaliana na ww.
    Nimetoka job lets say saa 11 jion,nimechoka, hasa my back andwaist, nianze kupika chapati, wali, kuku, samaki, mbogamboga, niandae juice, saladi, aje nimhudumie, sijui kucha, nywele, nguo, maji, nimuandalie nguo, nami pia, kisha maliza anikunjue the whole night na kesho yake 12 asubuhi nipo macho, monday to monday. Sijaweka malezi ye karen wangu six months old, Duu ii kitu ni ingine my dear?

    Out of topic
    A friend of mine atafanyiwa send off. ameniomba ushauri wa kitu gani atampatia huby to be wakati unapomtafuta yan pale ukumbini, hapendi akampatie mshumaa wala maua

    ReplyDelete
  3. ``Nakua mkweli leo. I have never lived na mwanamume maishani mwangu``

    woow woow!....babra is free... good news!

    gluv

    ReplyDelete
  4. Barbara Me huwa sijawahi kupita hapa kumbe mambo mazuri kama haya,ntakuwa nakuja kila siku.

    ReplyDelete
  5. I totally agree with u Barbra ila kiukweli u cannot do those mapishis everyday unless ni mama wa nyumbani...so I agree na mchangiaji wa kwanza kuwa sometimes hawa wanaume wanatakiwa waelewe hali halisi sio kila kukicha wanatafuta sababu za kuwa na nyumba ndogo...
    Ila kwa weekend au kama uko likizo you can definetly do that....

    ReplyDelete
  6. Mie nakubaliana na Barbara kuwa unyago mzuri ni yale mafunzo ya kila siku uliopewa na wazazi especially Mama (kwa sisi watoto wa kike) na siyo vitchen party vya masaa mawili!! Nikirudi kwenye mada; Cha muhimu ni kumpata huyo partner wako muelewa(Gentleman) hapo itakuwa haina shida. Lakini ukijipatia vingwendu hata upige tik tak za aina gani humo ndani no appreciation! Utahangaika na samaki wa kupaka, Mwenzio anazusha kingine!Mmmmmh.....Makubwa!!!

    Elmmy

    ReplyDelete
  7. Wote hapo na mwenye blog hamna utaalamu kuhusu maisha ya ndoa au kuishi na mwanaume.Hivyo vyote mlivyosema mi nafanyia na mme wangu na wote tunatoka kazi pamoja,ina maana nikatufute mapochopocho pembeni?

    ReplyDelete
  8. hongera b.hassan, topic zako nzuri..

    ReplyDelete
  9. Mdau wa 2 - hehehehhehe.. Sio lazima upike vyoooote hivyo nilivyotaja but at least chakula kizurii jamaniiii.. Anyway ni mtazamo wangu. About your friend - ngoja niangalie kesho ntakujibu.

    G luv hujatulia

    Mdau wa 4 - Karibu sanaaaaa and asante kwa kutembelea this blos. Waambie na wengine.

    Mdau wa 5 - Point taken ma...

    Elmmy - much love

    Mdau after Elmmy - sijakuelewa..

    Mdau wa mwisho - Thank u sana sanaaaa

    ReplyDelete
  10. Namaanisha topic kama hii wanatakiwa wachangie walio na uzoefu katika maisha hayo.Sio kila mtu analaumu wanaume.

    ReplyDelete
  11. Nina uzoefu wa hayo maisha(ndoa) wa zaidi ya miaka kumi! Hivyo naongea kutokana na exprerience yangu mwenyewe na watu wengine wengi tu. Ushauri; Mdada/Mkaka Sometimes, We should "agree to disagree"

    Elmmy

    ReplyDelete
  12. Barbara mi sijaelewa huo mchuzi unakuaje au ni mchuzi wa nn plz nijuze mwenzio

    ReplyDelete
  13. breathing timе in tantric massageThe second tip іѕ tгeat various
    аilments frοm migraines to агthritis
    аnd beyοnd.

    Check out my webpage: sensual massage In london Photos

    ReplyDelete

 

Sample text

Sample Text

Sample Text